Star Tv

Kufuatia  migogoro  kushamiri kati ya wachimbaji wadogo na uongozi wa kitengo cha ukaguzi na usalama wa mgodi wa Ikuzi wilayani Bukombe ambapo Mkuu wa Wilaya  hiyo  Ndugu, Said Nkumba alitoa siku tatu kuhakikisha  Bodi ya ushirika inamuondoa  Inspekta mkuu ndugu, Said Manumbu anayelalamikiwa  kwa Rushwa ,Bodi ya Ushirika imetengua uongozi wote na kuchangua  viongozi wapya kutekeleza Agizo la Mkuu wa Wilaya.

 

Mwenyekiti wa  chama cha Ushirika  wachimba madini ya dhahabu Ikuzi  Elias Andrea  ameongoza  Kikao  cha Bodi ya Ushirika ili kutekeleza agizo la Mkuu wa wilaya  alilowapa  kwamba ndani ya siku tatu wawe wameshachagua inspekta mkuu mwingine na kuhakikisha migogoro katika Rashi hiyo inakoma  nakufikia mwisho.

Jumla ya mainspekta 20 walioomba  nafasi hiyo na  baada ya kufanya uchaguzi  katibu  wa ushirika huo  Stanslaus Mkwavi akamtangaza Frank Buhuru  kuwa Mkaguzi  mkuu atakayeongoza idara  hiyo.

Baada ya matokeo hayo mwenyekiti wa ushirika huo Elias  Andrea  akawaasa waliochaguliwa na kutoa angalizo.

Uchaguzi huo umefanyika chini ya uangalizi wa katibu tarafa ya Siloka ,uongozi wa kijiji cha Ikuzi wa serikali.

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.