Star Tv

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli leo tarehe 21 Machi, 2019 amekutana na kufanya mazungumzo na Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Mambo ya Nje wa Qatar Mhe. Sheikh Mohammed bin Abdulrahman J.A. Al Thani, Ikulu Jijini Dar es Salaam.

Viongozi hao wamezungumzia uhusiano na ushirikiano mzuri uliopo kati ya Tanzania na Qatar na dhamira yao ya kuhakikisha uhusiano na ushirikiano huo unaendelezwa na kukuzwa zaidi hususani katika masuala ya uwekezaji katika gesi, madini, utalii na miundombinu ya barabara, bandari, nishati, reli na huduma za kijamii.

Mhe. Rais Magufuli amemshukuru Mhe. Sheikh Mohammed kwa kuja kwake hapa nchini pamoja ujumbe wa wawekezaji wenye dhamira ya kuwekeza nchini Tanzania na amemuomba ampelekee salamu za shukrani kwa Mtawala wa Taifa la Qatar Sheikh Tamim bin Hamad Al Thani kwa kuendeleza uhusiano na Tanzania.

Mhe. Rais Magufuli amesema Tanzania inazo fursa nyingi za uwekezaji zikiwemo uchakataji wa gesi, madini, utalii na usafiri wa anga hivyo amemuomba Sheikh Mohammed kuwahamasisha wafanyabiashara wa Qatar kushirikiana na Tanzania kuwekeza katika maeneo hayo.

Aidha, Mhe. Rais Magufuli ameiomba Qatar kushirikiana na Serikali ya Tanzania katika utekelezaji wa miradi mikubwa ya maendeleo ikiwemo uzalishaji wa nishati ya umeme, ujenzi wa reli, barabara na madaraja na pia amemualika Mtawala wa Qatar Sheikh Tamim bin Hamad Al Thani kufanya ziara hapa Tanzania.

Kwa upande wake Naibu Waziri Mkuu wa Qatar Sheikh Mohammed amemshukuru Mhe. Rais Magufuli na Serikali yake kwa kuendelea kushirikiana na Qatar katika masuala mbalimbali na kubainisha kuwa Qatar inathamini uhusiano huo.

Sheikh Mohammed ameahidi kuwa Qatar ipo tayari kufanyia kazi maombi yaliyotolewa na Mhe. Rais Magufuli na pia kuzileta kampuni za nchi hiyo kuja kuwekeza katika maeneo yenye fursa zenye manufaa kwa pande zote mbili.

Nae Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Prof. Palamagamba Kabudi amesema baada ya kukutana na Mhe. Rais Magufuli, yeye na Sheikh Mohammed watakua na mazungumzo ya kina kuhusu maeneo ya ushirikiano.

Mazungumzo ya viongozi hao yamehudhuriwa na Balozi wa Tanzania nchini Qatar Mhe. Fatma Rajab na Balozi wa Qatar nchini Tanzania Mhe. Abdullah Jassim Mohammed Al Medadi.

Chanzo; Ikulu

 

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.