Rais Dokta John Magufuli aagiza flyover ya Mfugale iliyopo makutano ya Tazara ifungwe kamera haraka ili watakao sababisha ajali wawe wanajulikana huku akisisitiza umuhimu wa daraja hilo kutunzwa vizuri.
Rais Magufuli amesisitiza umuhimu wa watanzania kulinda miundombinu hiyo na kubwa zaidi kuhakikisha haiwi sehemu ya kusababisha ajali. Kwa upande wake Afisa mtendaja Mkuu wa Tanroads Bwana Patrick Mfugale amesema serikali inatarajia kujenga daraja lingine la juu katika eneo la Chang'ombe, lengo likiwa ni kupunguza misongamano na kusababisha wananchi kuchelewa kufika katika shughuli zao mbalimbali.