Star Tv

Polisi mkoa wa Dodoma linamshikilia John Mwaisango kwa tuhuma za mauaji ya Mhadhiri wa chuo Kikuu cha dodoma Rose Malifred Mndenye ambaye alikuwa ni mke wake katika tukio lililotokea Mei 25 Mwaka huu na kwamba kwa sasa anatarajiwa kufikishwa mahakamani.

Kwa mujibu wa Kamanda wa polisi mkoani hapa Kamishna msaidizi mwandamizi wa polisi Gilles Muroto mtuhumiwa huyo amekamatwa akiwa mafichoni katika kijiji cha Chiwachiwa kata ya Mbingu wilaya ya Ifakara mkoani wa Morogoro.

Katika hatua nyingine Jeshi la polisi mkoani Dodoma linawashikilia watuhumiwa saba kwa kosa la kujihusisha na usafirishaji wa nyara za serikali kinyume cha sheria ya nchi.

Akitoa taarifa hiyo kamanda wa polisi kamishina msaidizi mwandamizi wa polisi Gilles Muruto amesema watuhumiwa hao wamekutwa na Kobe 536 ambao kati yao kobe 244 ni aina ya Pan Cake na kobe 366 ni aina ya Leopard wenye thamani ya zaidi ya shilingi Mil 84 Za kitanzania.

Amesema watuhumiwa hao wamekuwa wakikusanya wanyama pori hao kutoka maeneo mbali mbali ya nchi na kuwaleta mkoani Dodoma ambapo huandaliwa na kusafirishwa nje ya nchi .

Aidha kwa mara nyingine, jeshi la polisi linamshikilia msanii wa muziki wa kizazi kipya Rashid Abdalah maarufu kama chidbeenz mwenye miaka 33 mkazi wa Ilala Dar Es Saalam kwa kosa la kukutwa na dawa Za kulevya aina ya bhangi Hii ni mara ya pili kwa msanii huyo kushikiliwa na jeshi la polisi kwa tuhuma za kukutwa na dawa za kulevya.

Picha na mtandao

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.