Star Tv

Mzunguko wa siku za hedhi kwa wanawake ni jambo ambalo huwa halizungumzwi hadharani katika jamii nyingi barani Afrika kutokana na imani za kidini na kitamaduni.

Vivyo hivyo ushiriki wa wanaume katika suala la hedhi kwa msichana nchini Tanzania lina pande mbili, baadhi wanaunga mkono na wengine wanapingana nayo na kuona kwamba ni suala la siri.

Licha ya kuepo kwa kwa kampeni na harakati nyingi hivi karibuni katika shule na vyombo vya habari bado muamko ni mdogo.

Kampeni hizi zinaibua hisia tofauti miongoni mwa jamii wapo ambao wanachukizwa wakiamini kuwa si jambo sahihi kuzungumzia suala la hedhi hadharani kwasababu tu ya tamaduni kitu ambacho kwa namna moja au nyingine husalia kama kizingiti katika harakati za kuleta uelewa juu ya hedhi hasa kwa vijana.

Wasichana wengi wa sekondari wanakumbana na changamoto kubwa ambayo inaadhiri masomo yao na kufifisha ndoto zao kutokana na kutokuwa katika mazingira mazuri yanayowafanya wawe na hedhi salama.

Maji safi na salama, matundu ya vyoo vya kutosha, walimu walezi wanaojali, bajeti ya kuwezesha shule kununua pedi kwa ajili ya wanafunzi vyote hivyo ni changamoto kwao.

Halima Mohamed kutoka Taasisi ya TAI- Tanzania inayotoa elimu ya hedhi kwa vijana ni muhamasishaji ambaye anahamasisha watu kuchangia pedi huzikusanya na wanazipeleka kwenye shule mbalimbali anasema zoezi hilo linachukua muda mrefu kwa sababu muitikio bado ni mdogo.

Wakati Doreen Temba yeye pia anashiriki katika kutoa pedi bure shuleni,anasema waliamua kufanya shughuli hiyo ili kueza kuwabakiza watoto wa kike shuleni maana huwa wanajisikia aibu kutokana na kukosa kitu cha kujistiri,zamani walikuwa wanatumia khanga,vitenge ambazo zilikuwa hazisaidii.

Hata hivyo sio wanaume wote ambao wamekuwa pembeni katika harakati hizo,Kwa upande wake Kambarage Kasoga anaona kwamba hali hiyo ya hedhi sio jambo la ajabu na jamii anapaswa kutambua kuwa hilo ni jambo la kawaida tu, kwa kuwa kwenye familia au shuleni watoto wa kike wanahitaji msaada kutoka kwa baba na mwalimu pia hata wa kiume.

Huku dunia ikiwa inaadhimisha siku ya hedhi salama,wasichana wanakosa masomo 50 kati ya 194,vipindi 400 kati ya 1552 kwa mwaka kwa mujibu wa takwimu za tafiti zilizofanywa na Mtandao wa jinsia Tanzania(TGNP).

Kwa hisani ya BBC

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.