Star Tv

Naibu Spika Tulia Ackson amewaongoza waombolezaji Jijini Dar Es Salaam katika kuuaga mwili wa Mke wa Naibu waziri Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira Kangi Lugola, ACP Mary Lugola .

Vilio na simanzi vilitatawala nyumbani kwa Naibu waziri kangi Lugola mara baada ya kuanza kwa zoezi la kuuaga mwili wa marehemu.

Ndipo ukafika wakati wa kiongozi wa Bunge kuongea katika msiba huo naibu Spika Dkt Tulia Ackson kwa niaba ya Bunge la Tanzania akasema mwenyezi Mungu umuita Mtu wake wakati wowote hivyo ni vyema tukatenda mema wakati wote.

Kwa huzuni kubwa mume wa marehemu Kangi Lugola akasimama nakuongea mbele ya waombolezaji akiwakumbusha binadamu kutojisahau kwa kupanga mipango binafsi kumbe mpangaji wa yote ni Mwenyezi Mungu.

Hatimaye Jeshi la polisi pamoja na Chama cha Mapinduzi kupitia wawakilishi wao wakatoa salamu za rambirambi.

Marehemu Mary Lugola Mpaka anafariki Dunia alikua ni Afisa Mnadhimu Polisi Reli amefariki tarehe 1 mwezi Januari kwa niaba ya familia alikua akisumbuliwa na shinikizo la damu,mwili wake umesafirishwa kutoka Jijiji Dar es salaam kwenda Mwibala wilayani Bunda Mkoani Mara kwa ajili ya Mazishi.

Picha na mtandao.

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.