Star Tv

Utelekezaji wa watoto kwa mabinti na wanawake na kuwaacha kuishi katika mazingira hatarishi imekuwa changamoto inayosababisha ongezeko la watoto wanaolelewa katika vituo vya kulelea watoto yatima.

Baadhi ya vituo vinadaiwa kukosa uwezo wa kuwalea kutokana na kuelemewa na idadi kubwa ya watoto.

Kituo cha Faraja Ophanage childrens home kinatunza watoto zaidi ya 200 waishio katika mazingira hatarishi ambapo 30 kati yao wanaishi na maambukizi ya Virusi vya Ukimwi huku changamoto kubwa ikiwa ni ukosefu wa lishe kwa watoto hawa.

Kupitia changamoto zinazowakabili watoto hawa wadau mbalimbali wanaona kuna umuhimu wa kuungana nao hasa katika msimu huu wa sikukuu kwa kuwapatia mahitaji ya vyakula

Miongoni mwa vitu vilivyotolewa na wadau hawa kwa ajili ya watoto wa kituo cha Faraja ni pamoja na mahindi,mafuta,mchele nguo sabuni huku wadau mbalimbali wakihimizwa kujitokeza kuungana na watoto hawa hasa katika kipindi hiki cha msimu wa sikukuu.

Picha na mtandao.

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.