Rais Samia Suluhu Hassan, leo Septemba 10, 2021 amemteua Dkt. Stergomena Tax kuwa Mbunge wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Taarifa iliyotolewa leo Ijumaa Septemba 10, 2021 na Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais Ikulu, Jaffar Haniu imesema Tax ameteuliwa kutoka kwenye nafasi kumi za wabunge wa kuteuliwa na Rais.
Kabla ya uteuzi huo alikuwa Katibu Mtendaji wa Jumuiya ya Maendeleo ya Nchi za Kusini mwa Afrika (SADC) ambaye amemaliza muda wake mwezi Agosti 2021.