Star Tv

Baada ya kinyang’anyiro cha uchaguzi wa udiwani nchi nzima kumalizika jana November 26, 2017 na chama cha ACT wazalendo kushindwa kupata hata kata moja ya ushindi, kiongozi wa chama hicho Zitto Kabwe ameongelea suala hilo.

Zitto amesema kuwa wao kama chama wamekubali matokea hayo na kwamba wapiga kura wameamua na wao wamekubaliana na hilo na kwa sasa wanafanya tathmini ya matokeo ya nchi nzima na baadaye watazungumza na wananchi.

Ameeleza pia kuwa uchaguzi huu ulikuwa fursa ya kuzungumza na wananchi na kufikisha ujumbe wao kwani kuzuiwa kwa mikutano ya hadhara kunawanyima fursa ya kufanya hivyo.

“Tutazienzi kwani ndio haki yetu. Tunajiandaa na chaguzi ndogo zinazokuja ikiwemo za Ubunge kwenye majimbo yaliyowazi. Tutatumia mafunzo tuliyoyapata kwenye chaguzi ndogo hizi kujipanga na chaguzi zinazokuja.” – Zitto Kabwe 

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.