Star Tv

Makamu wa Rais wa Tanzania amemuagiza Naibu Waziri Ofisi ya Rais Tamisemi Dkt. Festo Dugange kumsimamisha kazi Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Nanyumbu Hamis Dambaya ili kupisha uchunguzi kutoka vyombo husika.

Dkt. Mpango, amefika uamuzi huo leo Julai 24, 2021 mara baada ya kufanya ziara ya kushtukiza katika stendi ya Mabasi ya Mangaka iliopo Wilaya ya Nanyumbu mkoani Mtwara.

Makamu wa Rais amekasirishwa na uongozi wa Wilaya kufanya upotevu wa fedha usiolingana na matokeo ya ujenzi wa mradi huo.

Ujenzi wa majengo ya stendi hiyo umetumia Shilingi Bilioni 2.2 kiasi ambacho Makamu wa Rais amesema hakilingani na ujenzi huo.

“Unajua vitu vingine Mkurugenzi ukiona huwezi kazi hii awamu ya sita jiondoe mwenyewe, Kwasababu hili jengo la hii stendi halijatumia hizo zaidi ya Shilingi Bilioni mbili unazonitamkia....lakini nitakufuatilia mpaka hela ipatikane…alafu unasema uongo na hela za maskini hawa. Hizo hela zirejeshwe kwasababu kinachooneka ni wakandarasi wanachezea hili jengo, anza kushughulika naye”- Ameagiza Makamu wa Rais Dkt. Mpango.

Aidha, Dkt. Mpango amesema viongozi hawana budi kusimamia fedha za serikali zinazopelekwa katika maeneo yao ili kuwaletea maendeleo wananchi na si vinginevyo.

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.