Star Tv

Rais Samia Suluhu Hassani amewataka wanawake nchini kujenga utamaduni wa kujiamini kwakuwa ukombozi wa mwanamke unaanza na mwanamke mwenyewe hasa katika kuchangamkia fursa mbalimbali za kiuchumi zilizopo katika jamii.

Rais Samia ametoa wito huo ikiwa ni mwendelezo wake wa kuzungumza na makundi mbalimbali tangu apate dhamana ya kuliongoza taifa ambapo safari hii amezungumza na wanawake wa mkoa wa Dodoma kwa niaba ya wanawake wote hapa nchini.

Samia amesema kutokana na utekelezwaji wa usawa wa kijinsia ambao unatekelezwa duniani kote ndio umesaidia wanawake kuonekana wanaweza katika nyadhifa za juu za maamuzi.

''Mafanikio makubwa yamepatikana katika eneo hili na mfano halisi ni mimi niliyesimama hapa, miaka 20,25,30 nyuma hatukuwa tukilitazamia hili, lakini leo imewezekana tuko hapa….idadi ya wanawake katika vyombo vya maamuzi imeongezeka''- Rais Samia.

Amesema serikali imeendelea kuongeza fursa za wanawake kupata ajira na amewataka wananchi hao kuhakikisha nawanatumia fursa hizo vema ili mwanamke awe amekombolewa katika Nyanja ya kiuchumi.

Kuhusu matukio ya ukatili wa kijinsia Rais Samia Suluhu Hasan ametumia jukwaa hilo kuwataka wanawake kutumia vizuri wingi wao ili kupambana na vitendo hivyo ambavyo bado vinaonekana kuwa tatizo kubwa linalochangiwa na visasi na mani potofu.

Aidha, Rais Samia amemuelekeza Waziri wa Afya, Dkt. Dorothy Gwajima kuweka mpango mzuri wa ndugu kulipa deni la hospitali ili ikitokea mgonjwa wao amefariki dunia wakati akitibiwa, maiti isizuiwe.

Amesema si sawa maiti kuzuiwa na kwamba ni muhimu ukawekwa utaratibu wa kulipa deni la matibabu wakati taratibu za msiba zikiendelea.

“Hili la Watu kudaiwa wakati mtu amefariki wekeni mpango vizuri, hata Kidini tunaambiwa mtu akidaiwa hazikwi mpaka deni lilipwe ila sio kwa deni la Serikali, haileti maana mtu amefiwa anawaza msiba, kusafirisha na kuzika halafu bado unazuia maiti, hili haliwezekani.Nakuelekeza Waziri hebu nendeni mkaweke mpango mzuri wa kulipa deni na sio kuzuia maiti.”-Samia

Aidha, kupitia kauli yake hiyo Rais Samia Amefafanua kuwa tamko lake la maiti kutozuiwa lisichukuliwe vibaya; “Wananchi muelewe sio kwamba deni lisilipwe bali uwekwe mpango mzuri na mmoja wapo ni kulipa wakati matibabu yakiendelea na muhimu zaidi ni kuwa na bima ya afya,”- Amesema Rais Samia.

Mkutano huo wa wanawake umeenda sambamba na kauli mbiu isemayo “Mwanamke ni nguzo ya maendeleo tujitambue, tujizatiti tutekeleze wajibu wetu”, ambao umehudhuriwa na viongozi mbalimbali wa serikali, wanawake kutoka Tanzania Bara na Visiwani.

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.