Star Tv

Mtanzania Rashid Charles Mberesero aliyehukumiwa kifungo cha maisha mwaka 2019 baada ya kupatikana na hatia ya kushiriki shambulizi la kigaidi mnamo 2015, amejitia kitanzi katika gereza la Kamiti.

Msemaji wa idara ya magereza Kennedy Aluda jana Jumapili Nov 29,2020 alivieleza vyombo vya habari nchini Kenya kwamba, Bwana Mberesero alipatikana amejinyonga gereza namba 24 kwenye jumba la H.

“Alitumia blanketi kama kamba na kujinyonga. Mwili wake ulipatika ukining’inia kupitia dirishani ukiwa na blanketi shingoni”- alisema Bwana Aluda.

Aidha, Msemaji idara ya Gereza amesema kuwa uchunguzi tayari umeanzishwa kubaini kilichomsukuma Mberesero kujitoa uhai, Hata hivyo, marehemu alikuwa na tatizo la kiakili na alikuwa akipokea matibabu mara kwa mara.

Taarifa ndani ya gereza hilo zilisema marehemu alidungwa sindano Alhamisi kabla ya kujiua siku iliyofuata saa nane mchana, lakini pia upasuaji wa maiti utafanywa kubaini chanzo kamili cha kifo chake.

“Uchunguzi huo hata hivyo lazima uhusishe familia yake iliyoko nchini Tanzania”- aliongeza Bw Aluda.

Bw Mberesero alikuwa akitumikia kifungo cha maisha baada ya kupatikana na hatia ya kushambulia Chuo cha Garissa mnamo Aprili 2015. Shambulizi hilo lilisababisha vifo vya watu 150 ambao wengi walikuwa wanafunzi huku wengine 100 wakijeruhiwa.

Polisi walisema Jumapili walipokea ripoti katika kituo cha polisi cha Kahawa Magharibi kutoka kwa afisa anayehusika na masuala ya usalama katika gereza la Kamiti kwamba kuna mahabusu aliyekuwa amejinyonga gerezani saa moja kasoro dakika 10 jioni.

“Maafisa wa polisi walitembelea gereza hilo nambari 24 kwenye jengo la H na wakapata mwili wa Rashid Charles Mberesero, raia wa Tanzania mwenye umri wa miaka 25 ukiwa umening’inia na umefungwa kwa blanketi shingoni na kwenye chuma cha dirisha”- ilibainisha ripoti kwenye kituo hicho cha polisi.

Marehemu alipatikana na hatia ya kupanga njama ya kutekeleza mashambulizi ya kigaidi na mahakama moja ya Nairobi mwaka 2019.

Alihukumiwa maisha lakini wenzake Mohamed Abdi Abikar na Hassan Aden Hassan wakapewa hukumu nyingine, Ambapo rekodi za mawasiliano kwenye simu na maandishi yalithibitisha watatu hao walihusika na shambulizi hilo la kigaidi.

 

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.