Star Tv

Chama cha wamiliki wa Mabasi ya abiria TABOA umekanusha kuwa hakutakua na mgomo wa kusafirisha abiria hapo kesho kama ilivyoripotiwa 

Taharuki kubwa imezuka baada ya kusambaa kwa taaarifa ya Video ikitangaza mgomo wa nchi nzima kupinga Kanuni mpya za leseni.

Akizungumza Jijini Dsm Mwekahazina wa TABOA Issa Nkya amesema ni kweli wanapinga kanuni hiyo lakini hakuna mgomo bali kuna mgogoro wa kisheria na Sumatra.

Nkya amesema Jumatano ya November 15 kutakua na kikao na Sumatra kujadili kanuni na baada ya hapo tamko litatolewa.

Kwa upande Mkurugenzi wa huduma za Sheria kutoka Sumatra Tumaini Silaa amesema kanuni zinazolalamikiwa hazina tatizo lolote shida ni kwamba TABOA bado hawajizielewa.

Silaa amesema Kwenye mkutano wa Jumatano watawaelimisha wadau kuhusu kanuni hiyo, huku akitoa onyo kwa Mmiliki wa mabasi atakaethubutu kugoma.

Kanuni inayopigiwa kelele na TABOA ni ile inayosema kuwa dereva akifanya kosa, ataadhibiwa kwa kupelekwa Mahakamni na mmiliki wa basi hilo atatozwa faini.

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.