Star Tv

Mkuu wa polisi nchini Inspekta Jenerali Simon Sirro amesema waliohusika na ajali ya moto iliyowaua watoto 10 wa shule ya msingi Byamungu Islamic iliyoko wilayani Kyerwa mkoani Kagera.

Kamanda Sirro wakati akizungumza na Waandishi wa Habari amebainisha kuwa shule hiyo ilikuwa na hitilafu nyingi zikiwemo namna ambavyo wayaringi ya jengo hilo imefanyika pamoja na matofali yaliyotumika kujengea shule hayakuwa imara.

''Kikubwa Hatujafahamu chanzo hasa ni nini, lakini kwa haraka inaonekana jengo halikuwa madhubuti, ndio maana tumemkamata mwenye shule. Lakini pia nimesema wamtafute Afisa Elimu na Wakaguzi wote waliokuwa wanakuja kukagua hii shule, walikuwa wanaona watoto wanakaa wapi?, jengo lilikuwa imara?, ni lazima hapa tuwe wakali kwasababu tayri maisha ya watu yamekwisha ondoka''-Amesema Kamanda Sirro.

Jumla ya wanafunzi 74 walikuwepo kwenye bweni wakati ajali ya moto ilipotokea ambapo mpaka sasa chanzo cha moto huo hakijajulikana.

Aidha, Kamanda Sirro amesema kuwa wanajaribu kutafuta vyanzo ikiwa ni pamoja na uwezekano wa adui wa nje kutumia mwanya kufanya jambo hilo, amewataka wakazi wa Kyerwa kushirikiana kutoa taarifa zozote juu ya chanzo cha ajali hiyo.

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.