Star Tv


Mafuriko yaliyotokea wiki hii nchini Afghanistan yamegharimu maisha ya karibu watu 160 na waokoaji wanaendelea kutafuta watu ambao wamekwama kwenye matope na chini ya vifusi vya nyumba zilizosombwa na maji, mamlaka imesema.

Mikoa kumi na tatu, hasa kaskazini mwa nchi, imeathirika, kulingana na wizara yenye dhamana ya kukabiliana na majanga.

Katika mkoa wa Parwan peke yake, kaskazini mwa Kabul, watu 116 wamepoteza maisha, zaidi ya 120 wamejeruhiwa na 15 bado hawajulikani waliko, viongozi wamesema.

Wizara ya ulinzi imebaini kwamba vikosi vya usalama vya Afghanistan vimekuwa vinasaidia katika shughuli ya uokoaji na kutoa misaada, licha ya kukabiliwa na ghasia zinazotekelezwa na Taliban nchini humo.

Wizara ya ulinzi imebaini kwamba vikosi vya usalama vya Afghanistan vimekuwa vinasaidia katika shughuli ya uokoaji na kutoa misaada, licha ya kukabiliwa na ghasia zinazotekelezwa na Taliban nchini humo.

Jumuiya ya kujihami ya nchi za Magharibi, NATO, imesema vikosi vyake vikilisaidia jeshi la Afghanistan vimepeleka chakula, maji na blanketi kwa maeneo yaliyoathiriwa.

 

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.