Star Tv

Maafisa wa afya wa jiji la Wuhan lililokuwa kitovu cha mlipuko wa janga la virusi vya corona wametangaza kutokuwa na mgonjwa yoyote aliyelazwa hospitalini kutokana na maradhi yanayosambazwa na virusi hivyo.

Taarifa ya Wuhan kutokuwa na mgonjwa wa COVID_19 imetolewa na msemaji wa tume ya kitaifa ya afya nchini China, Mi Feng aliyezungumza na waandishi wa habari hii leo.

Taarifa hii ya karibuni zaidi inaonyesha hakuna maambukizi yoyote ya virusi vya corona kwenye jiji hilo, na imepongeza hatua za pamoja kati ya Wuhan na wahudumu wa afya kutoka maeneo mbalimbali nchini humo.

Jiji hilo liliripoti juu ya watu 46,452 waliougua homa ya mapafu COVID-19 sawa na asilimia 56 ya maambukizi yote nchini China, ambapo watu 3,869 walifariki dunia.

 

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.