Star Tv

Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani Mike Pompeo amedai kuwa serikali za Urusi na China zinajiepusha kutoa taarifa sahihi za virusi vya  ugonjwa wa Corona.

Pompeo ameyasema hayo katika mahojiano ya kipindi cha redio cha 'Washington Watch' ambapo akikariri madai yake ya huko nyuma juu ya kucheleweshwa na China taarifa za ugonjwa huo wa virusi vya Corona, a,mbapo amesema kuwa hali hiyo inahatarisha maisha ya maelfu ya watu wengi duniani.


Kadhalika Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani ameendelea kudai kuwa Iran na Urusi pia zinatoa taarifa zisizo sahihi kuhusu virusi vya Corona.


Madai hayo ya Pompeo ni kutokana na radiamali kuhusu tuhuma zilizoelekezwa kwa Washington kwamba jeshi la Marekani ndio lililozalisha na kusambaza virusi vya Corona ambavyo vimeikumba pia chi hiyo.


Waziri huyo amesema kuwa serikali ya Washington iko chini ya mashinikizo makali ya ndani yanayosababishwa na usimamizi mbaya wa idara za kukabiliana na Corona.


Aidha Waziri Pompeo amenukuliwa akiendelea kutoa vitishokwa China kwamba baadaye Marekani itachukua uamuzi muhimu kuhusu uhusiano baina ya nchi hizo mbili (China na Marekani) utakavyokuwa.

                                Mwisho.

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.