Star Tv

Serikali mpya ya Tunisia itakayoongozwa na Waziri Mkuu Elyes Fakhfakh imekula kiapo mbele ya Rais wa nchi hiyo Kais Saied, huku Fakhfakh akiahidi kutatua matatizo ya wananchi wake.

Hafla ya kuapishwa baraza jipya la mawaziri la Tunisia ilifanyika jana baada ya bunge kuidhinisha baraza hilo lililopendekezwa na Waziri Mkuu Fakhfakh.

Bunge la Tunisia liliidhinisha serikali hiyo mpya kwa kura 129 za 'ndiyo' dhidi ya 77 za 'hapana'.

Wakati akiomba ridhaa ya bunge ya kulipitisha baraza la mawaziri alilopendekeza, Fakhfakh aliwaeleza wabunge katika kikao cha siku ya Jumatano cha bunge la nchi hiyo kuwa, atajitahidi kustawisha uchumi na kushughulikia matatizo ya wananchi.

Amesema kustawisha uchumi wa nchi hiyo na kutatua matatizo ya wananchi  wa Tunisia ndivyo vitakuwa miongoni mwa vipaumbele muhimu zaidi vitakavyofanyiwa kazi na serikali yake na akawataka wabunge, vyama vya siasa na asasi zote za kiraia nchini humo kuisaidia serikali katika suala hilo.

Hali mbaya ya uchumi hususani tatizo la ukosefu wa ajira ni miongoni mwa matatizo muhimu zaidi yanayoikabili Tunisia kwa sasa, kiasi kwamba katika miaka ya karibuni nchi hiyo imeshuhudia maandamano kadhaa ya kupinga serikali.

                                  Mwisho.

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.