Mshirika wa muda mrefu wa Rais wa Marekani, Donald, Trump ajulikanaye kwa jina la Roger Stone amehukumiwa kifungo cha miezi 40 jela.
Stone amehukumiwa adhabu hiyo baada ya kupatikana na hatia ya kuwadanganya wachunguzi na kuzuia sheria kuchukua mkondo wake katika uchunguzi kuhusu Urusi kuingilia uchaguzi wa urais nchini Marekani mwaka 2016.
Jaji Amy Berman Jackson wa mahakama ya Marekani, amesema udanganyifu uliofanywa na Stone unatishia demokrasia ya nchi hiyo.
Hukumu hiyo imetolewa baada ya mwanasheria mkuu wa Marekani, William Barr kupunguza hukumu yake iliyopendekezwa kwa Bwana Stone ya miaka saba gerezani.
Mawakili wa Stone wameomba mteja wao awe chini ya uangalizi wa mahakama badala ya kutumikia kifungo chake gerezani, kwa kuzingatia umri wake ambao ni miaka 67, afya yake na kwa kuwa hana historia ya uhalifu.
Mwisho