Star Tv

Rais wa Uturuki Recep Tayyip Erdogan ametishia kumchukulia hatua za kijeshi mbabe wa kivita nchini Libya, Khalifa Haftar, wakati akizungumza na wabunge wa chama  chake ikiwa ataendelea kuishambulia serikali ya mjini Tripoli inayotambuliwa kimataifa.

Haya yamejiri baada ya Haftar kuondoka katika mkutano wa upatanishi mjini Moscow hapo jana, bila kusaini makubalino ya kusitisha mapigano, ambayo kiongozi wa serikali ya mjini Tripoli ameyaridhia.

Rais Erdogan amesema atashiriki katika mkutano mwingine kuhusu amani nchini Libya, ambao utafanyika Jumapili ijayo mjini Berlin, Ujerumani, ukizishirikisha pia nchi za Ufaransa, Uingereza na Italia, na mataifa ya kiarabu kama Misri, Algeria na Umoja wa Falme za Kiarabu.

Aidha, Uturuki imepeleka vikosi nchini Libya kuiimarisha serikali ya waziri mkuu Fayez al-Sarraj, na Rais Erdogan amesema vitabaki huko mpaka utulivu utakapopatikana nchini humo.

                                                                                               Mwisho.

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.