Star Tv

Brussels:Viongozi wa Ulaya wanafanya kikao cha faragha leo kujadili kuhusu nyadhifa kuu za Umoja wa Ulaya, wakati mirengo pinzani katika bunge jipya la umoja huo ikijaribu kuunda mrengo wa siasa za wastani wenye viti vingi.

Uchaguzi wa mwezi uliopita barani Ulaya ulishuhudia vyama vinavyounga mkono sera za Umoja wa Ulaya na vya siasa za wastani za mrengo wa kushoto vikipambana kuhimili kishindo cha siasa kali za kizalendo, lakini hilo likawaacha viongozi wao wakiwa wametofautiana hata zaidi. Wadhifa unaogombaniwa ni wa mrithi wa Jean Claude Juncker kama Rais wa Halmashauri Kuu ya Ulaya ambayo ndio taasisi yenye mamlaka makubwa ya Umoja wa Ulaya. Rais wa Baraza la Ulaya Donald Tusk anaongoza juhudi za viongozi hao kumtuewa mgombea kabla ya mkutano ujao wa kilele mnamo Juni 20 na 21, lakini dalili za mapema zinaonesha kuwa mazungumzo hayo yatakuwa marefu na magumu.

CHANZO: Idhaa ya Kiswahili DW

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.