Star Tv

Familia za wahanga wa mauaji ya Tiananmen nchini China wamefanya kumbukumbu ya miaka 30 tangu ukandamizaji huo wa vuguvugu la demokrasia ulipofanyika.

Familia hizo zimeitaka serikali ya China kukubali yaliyotokea na kuwaadhibu waliohusika. Kiongozi wa wanafunzi, Wu'er Kaixi ametoa wito wa vikwazo vya kimataifa dhidi ya tabaka la viongozi wa kikomunisti wa China. Watu wengi waliuawa Juni 4 mwaka 1989, pale jeshi la China lilipotumia vifaru dhidi ya wanafunzi waliokuwa wakidai mabadiliko na demokrasia zaidi katika viwanja vya Tiananmen. Umoja wa Ulaya umetoa wito wa kuwepo uchunguzi wenye uwazi kuhusu mauaji hayo, nayo Marekani imeelezea mshikamano na familia ambazo bado zinaomboleza wapendwa wao waliopoteza maisha katika ukandamizaji huo. China inasema miito ya pande hizo ni kisingizio cha kuingilia katika mambo yake ya ndani.

CHANZO: Idhaa ya Kiswahili DW

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.