Star Tv

Leo ni Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari Duniani, ambapo Umoja wa Mataifa umetumia siku hii kuwatunuku waandishi wawili wa shirika la habari la Reuters wanaotumikia kifungo cha miaka saba nchini Myanmar tuzo ya juu kabisa ya uhuru wa vyombo vya habari.

Wa Lone na Kyaw Soe Oo wametunukiwa tuzo katika mkesha wa maadhimisho ya siku hii, ambayo mwaka huu yanafanyika kimataifa nchini Ethiopia. Shirika la Elimu, Sayansi na Utamaduni la Umoja wa Mataifa (UNESCO) liliikabidhi Tuzo ya Uhuru wa Habari ya Guillermo Cano kwa Thura Aung, kaka yake Wa Lone, wakati wa sherehe hizo usiku wa kuamkia leo mjini Addis Ababa. Waandishi hao wawili walikamatwa mwishoni mwa mwaka 2017 wakati wakichunguza operesheni ya kijeshi na uvunjaji wa haki za binaadamu, yakiwemo mauaji ya kiholela, nchini Myanmar. Baadaye walitiwa hatiani kwa kuvunja Sheria ya Siri za Serikali. Umoja wa Mataifa na makundi mengine ya haki za binaadamu wamekuwa wakiishutumu serikali ya Myanmar kwa kuendesha kampeni ya kuwaangamiza Waislamu wa jamii ya Rohingya.

CHANZO: Idhaa ya Kiswahili DW

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.