Star Tv

Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Watoto (UNICEF) limetoa ripoti inayoeleza kupungua kwa kesi za mimba katika umri mdogo duniani kote.

Shirika hilo limeeleza kuwa takriban ndoa za utotoni Milioni 25 zimezuiwa katika kipindi cha miaka 10 iliyopita ambapo kwa sasa mtoto mmoja kati ya watano wanaolewa kabla ya umri wa miaka 18 ukilinganisha na mmoja kati ya wanne aliyekuwa anaolewa kipindi hicho. Nchi za kusini mwa Bara la Asia pia zimepunguza ndoa za utotoni huku Afrika ikiendelea pia kujitahidi kukabiliana na tatizo hilo ambapo kwa nchi kama Ethiopia imepunguza tatizo hilo kwa theluthi. Ripoti hiyo inaeleza kuwa mzigo wa ndoa za utotoni unaendelea kuzilemea nchi za Kusini mwa Jangwa la Sahara, ambako jitihada zaidi zinahitajika ili kuondoa tatizo hilo kabisa. UNICEF inasema kuwa mmoja kati ya watoto watatu wanapitia ndoa za utotoni kwa kipindi hiki Afrika ukilinganisha na mmoja kati ya watoto watano waliokuwa wakiolewa miaka kumi iliyopita. Viongozi wa dunia wameapa kumaliza tatizo la ndoa za utotoni ifikapo mwaka 2030 chini ya Malengo Endelevu ya Umoja wa Mataifa (SDGs).

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.