Star Tv

Gari moja lililokuwa linaendeshwa kwa kasi katika jimbo la California liliruka na kuingia ndani ya ghorofa ya juu kwenye jumba moja baada ya kugonga uzio wa kutenganisha barabara, taarifa zinasema.

Ajali hiyo, ambapo sehemu moja ya gari ilibaki ikining'inia nje ya jengo hilo, ilitokea mapema Jumapili asubuhi.

Watu wawili waliokuwa ndani ya gari hilo walinusurika na majeraha madogo, kwa mujibu wa polisi.

Polisi wameambia wanahabari kwamba dereva wa gari hilo anadaiwa kutumia dawa na alikuwa ametembelea hospitali moja.

Mmoja wa wawili hao alifanikiwa kujitoa kutoka kwenye gari hilo lakini huyo mwingine alikwama kwa zaidi ya saa moja hadi maafisa wa uokoaji walipofika.

Ajali hiyo pia ilisababisha kuzuka kwa moto mdogo ambayo wazimamoto walifanikiwa kuuzima.

Wazimamoto walipakia picha za kisa hicho na walikuwa wanawapata watu yaliyokuwa yakijiri siku yote..Kisa hicho kilitokea Santa Ana, maili 35 (56km) kusini mwa Los Angeles.

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.