Rais wa Uganda Yoweri Museveni ametishia kuyaondoa majeshi ya nchi yake katika mpango wa usalama nchini Somalia.
Akizungumza na chombo cha habari cha Ufaransa ‘France 24’ Rais Museveni amejibu swali aliloulizwa kuhusu mpango wake wa kuondoa majeshi yake ya UPDF nchini Somalia baada ya ongezeko la mashambulizi kutoka kwenye kundi la waasi la Al-Shabab pamoja na mgogoro wa kisiasa nhini humo.
Akielezea mgogoro wa kisiasa nchini Somalia mwaka 2011, Museveni alitaka maelewano ambayo yalipelekea kujiuzulu kwa aliyekuwa Waziri Mkuu kipindi hicho Mohamed Abdullahi Farmaajo ambaye kwa sasa anahudumu kama Rais na katika kipindi hicho Museveni alitishia kuondoa majeshi yake.
Uganda inakuwa nchi ya kwanza kupeleka majeshi yake nchini Somalia kupitia mwamvuli wa kulinda amani Afrika wa mwaka 2007.
Museveni akielezea juu ya msimamo wake alisema kuwa hana imani sana majeshi yanayotoka nje ya Afrika lakini kutokana na kwamba kazi inayopaswa kufanywa ni kubwa basi hakukuwa na muda kushikilia maneno yake.
Amesema kuwa, maamuzi ya kujiondoa kwa majeshi yake yanaweza kufuata utaratibu wa mazungumzo na Umoja wa Afrika lakini ameona ni muda sasa wa wao wajilinde wenyewe.
Siku ya jumatatu, majibizano baina ya Rais na Waziri Mkuu wa Somalia yameendelea baada tu ya kufukuzwa kazi mkuu wa kitengo cha usalama wa taifa.
Hata hivyo, inawezekana uchaguzi uliopangwa kufanyika mwishoni mwa mwezi Oktoba mwaka huu ukasogezwa mbele baada ya uchaguzi wa wabunge kupelekwa mbele mwisho wa mwezi Novemba.