Star Tv

Mlipuko wa ugonjwa wa uti wa mgongo au meningitis umetangazwa kuua watu 120 Kaskazini mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo.

Imethibitishwa kuwa mpaka sasa watu zaidi ya 120 wamekufa kutokana na ugonjwa huo.

Mgonjwa wa kwanza nchini DRC aliripotiwa Julai.

Mlipuko huo umekuwa mgumu kukabiliana nao kwa kuwa jamii inauhusisha na uchawi, shirika la afya duniani (WHO) limeiambia BBC.

Sampuli zilizotumwa Ufaransa zimebaini kuwa bakteria wanaohusika na mlipuko huo wanaweza kusababisha janga kubwa.

Watu wengi wamekufa na jamii inapaswa kulaumiwa kwa kushindwa kuwajibika, kwakuwa badala ya kutafuta tiba, baadhi ya watu wamekuwa wakitoka sehemu moja kwenda nyingine wakiwa na matumaini kuwa ugonjwa huo hautawafuata.

Serikali ya DRC na WHO wametuma vikosi vya watumishi wa afya kaskazini mashariki mwa jimbo la Tshopo ili kukabiliana na hali hiyo.

 

 

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.