Mlipuko wa ugonjwa wa uti wa mgongo au meningitis umetangazwa kuua watu 120 Kaskazini mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo.
Imethibitishwa kuwa mpaka sasa watu zaidi ya 120 wamekufa kutokana na ugonjwa huo.
Mgonjwa wa kwanza nchini DRC aliripotiwa Julai.
Mlipuko huo umekuwa mgumu kukabiliana nao kwa kuwa jamii inauhusisha na uchawi, shirika la afya duniani (WHO) limeiambia BBC.
Sampuli zilizotumwa Ufaransa zimebaini kuwa bakteria wanaohusika na mlipuko huo wanaweza kusababisha janga kubwa.
Watu wengi wamekufa na jamii inapaswa kulaumiwa kwa kushindwa kuwajibika, kwakuwa badala ya kutafuta tiba, baadhi ya watu wamekuwa wakitoka sehemu moja kwenda nyingine wakiwa na matumaini kuwa ugonjwa huo hautawafuata.
Serikali ya DRC na WHO wametuma vikosi vya watumishi wa afya kaskazini mashariki mwa jimbo la Tshopo ili kukabiliana na hali hiyo.