Kundi la Wanamgambo wa Taliban limewazuia Wamarekani wanaoingia uwanja wa ndege wakati ndege ya Marekani inaondoka Afghanistan, ambapo bado kulikuwa na raia wa Marekani na Waafghani waliokuwa wakitarajia kuondoka na walikuwa wakijaribu kuingia kwenye uwanja wa ndege, maafisa wameeleza.
Katika mkutano wa waandishi wa habari awali, Jeneali McKenzie, Mkuu wa vikosi vya Marekani alithibitisha kuwa kuna Wamarekani 100-250 ambao wameshindwa kufika uwanja wa ndege au wameshindwa kuingia kwenye ndege.
Mwanajeshi wa zamani wa Marekani ambaye amesema kuwa alikuwa akisaidia kuratibu shughuli za uokoaji akiwa katika makazi yake Connectcut amesema Taliban waliwazuia wengi kupita. Alikuwa akiwasiliana na wengi, aliandika katika ukurasa wa twitter.
''Taliban walikuwa hawawezekani kuratibu nao mpaka mwisho. Walikataa kutoa ushirikiano nje ya milango ya kuingilia,''- Alisema.
Alex Plitsas, Mwanajeshi wa zamani amesema bado anawasiliana na Wamarekani wanaotaka kuondoka Afghanistan, lakini baadhi hawajajisajili kwenye mamlaka za Marekani, ''Hatuwezi kuwaokoa watu ambao hatujui kama wako huko,'' Alibainisha mwanajeshi huyo wa zamani.
#ChanzoBBCSwahili