Star Tv

Afrika Kusini imepeleka jeshi kukabiliana na ghasia zilizotokea baada ya kufungwa kwa Rais wa zamani wa taifa hilo Jacob Zuma.

Maduka yalivamiwa na majengo yalichomwa moto siku ya Jumatatu, wakati Zuma akisikiliza kesi yake katika mahakama ya juu.

Watu wapatao sita wameuawa na 200 kukamatwa tangu ghasia hizo zianze wiki iliyopita.

Zuma amehukumiwa kwa kosa la kuidharau mahakama baada ya kushindwa kuhudhuria kesi yake ya madai ya rushwa wakati wa utawala wake.

Zuma mwenye umri wa miaka 79, ambaye alikanusha kuhusika katika madai ya rushwa, lakini alienda mwenyewe polisi wiki iliyopita ili kuanza kifungo chake cha miezi 15.

Kesi hiyo imeibua matukio ambayo hayakutarajiwa nchini humo ambapo hawajawahi kushuhudia kuona Rais wa zamani akifungwa gerezani.

Jumatatu hii Julai 12, 2021 picha za video zilionesha maduka makubwa yakichomwa moto katika mji wa Pietermaritzburg, katika eneo alikotokea Zuma, KwaZulu-Natal, na watu wakifanya maandamano.

Jumapili waandamanaji walionekana wakiandamana katika maeneo ya biashara ya mjini Johannesburg.

Jeshi limesema limeagizwa kwenda kusaidia kupunguza ghasia ambazo zimekuwa zikiendelea kwa siku kadhaa.

Rais Cyril Ramaphosa amesisitiza raia wanaoandamana kuwa na utulivu akisema hakuna maelezo juu ya vurugu hizo.

Zuma alikamatwa kawa kukaidi maelezo ya kutoa ushaidi juu ya kesi ya rushwa ilyokuwa inamkabili wakati yuko madarakani.

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.