Star Tv

Rais mteule wa Marekani Joe Biden aliwasili Washington katika mkesha wa sherehe ya kuapishwa kwake, wakati mtangulizi wake Donald Trump ambaye atasusia hafla hiyo ya kula kiapo kwa mara ya kwanza akiitakia mafanikio serikali mpya.

Machozi yalimtoka Biden katika sherehe ya kuagwa mjini Wilmington, Delaware, ambako alitoa heshima kwa marehemu mwanawe wa kiume kabla ya kupanda ndege kuelekea katika mji mkuu.

Kwa upande wake, Trump ambaye hajaonekana hadharani kwa wiki moja sasa, alivunja ukimya wake wa siku nyingi kupitia hotuba iliyorikodiwa kwenye mkanda wa video.

Trump kwa mara ya kwanza aliiwaomba Wamarekani ''kuiombea'' mafanikio serikali ijayo ya Biden, ikiwa ni mabadiliko ya msimamo wa wiki nyingi alizotumia kuishawishi idadi kubwa ya wafuasi wake wa Republican kuwa Biden alifanya udanganyifu katika kinyang’yiro cha urais.

Chanzo na DW.

 

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.