Star Tv

Aliyekuwa rais wa Sudan Omar al-Bashir alionekana hadharani jana Jumapili, kwa mara ya kwanza tangu kupinduliwa na jeshi Aprili 11.

Bashir alisafirishwa kutoka gereza la Kober mjini Khartoum hadi ofisi ya mwendesha mashtaka kukabiliana na shutuma za ufisadi. Mwendeshamashtaka Alaeddin Dafallah aliwaambia waandishi wa habari kwamba kiongozi huyo wa zamani anashtakiwa kumiliki fedha za kigeni kinyume cha sheria, ubadhirifu na kupokea zawadi kwa njia zisizo halali. Utawala wa miongo mitatu wa Bashir uliangushwa na jeshi baada ya maandamanano ya miezi kadhaa, kupinga kupanda kwa bei ya chakula na kudhoofika kwa uchumi. Mwezi Mei alishtakiwa kuhusika katika mauaji dhidi ya waandamanaji, na polisi ilisema ilikuta nyumbani kwake fedha taslimu katika sarafu mbali mbali, zenye thamani jumla ya dola milioni 100 za kimarekani.

CHANZO: Idhaa ya Kiswahili DW

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.