Star Tv

Raia wa Misri wanapiga kura ya maoni leo inayolenga kumpa nguvu zaidi Rais Abdel Fattah al-Sisi.

Kura hiyo iliyopingwa na makundi ya haki za binaadamu, inatazamiwa kuridhia mabadiliko makubwa ya kikatiba ambayo yataongeza muhula wa al-Sisi madarakani hadi mwaka 2024. Mbali ya hilo, kura hiyo pia itampa al-Sisi, mwenye umri wa miaka 64, nafasi ya kuwania tena kwa miaka sita baadaye, madaraka zaidi juu ya mahakama, na nguvu kubwa kwa jeshi kushiriki siasa. Bunge tayari limeshapiga kura wiki hii na kuunga mkono mabadiliko hayo, ikiwa ni pamoja na kurefusha muhula wa urais kutoka miaka minne hadi sita.

CHANZO:Idhaa ya Kiswahili DW

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.