Star Tv

Bunge la Algeria litamchagua Rais mpya wa mpito wiki ijayo. Kwa mujibu wa shirika la habari la serikali -APS- zoezi hilo litafanyikakutokana na rais mkongwe Abdelaziz Bouteflika kujiuzulu kufuatia maandamano ya umma dhidi yake.

Bouteflika iliukatisha utawala wake wa miaka 20 baada ya jeshi kuacha kumuunga mkono tena, kufuatia maandamano ya wiki sita na miito ya kutaka mageuzi ya kidemokrasia nchini Algeria. Mwenyekiti wa sasa wa baraza la juu la bunge Abdelkader Bensalah huenda akateuliwa kushikilia wadhifa huo. Lakini Bensalah, sawa na Waziri Mkuu Nouredine Bedoui na Tayeb Belaiz, mkuu wa Baraza la Katiba wanakabiliwa na shinikizo la kuondoka kutoka kwa waandamanaji ambao wanawatazama kama watu wa karibu na mfumo wa sasa.

CHANZO: Idhaa ya Kiswahili DW

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.