Star Tv
Msumbuji imeanza leo siku tatu za maombolezi ya kitaifa baada ya kimbunga kikali kilichoandamana na mafuriko kuwauwa mamia ya watu na kusababisha uharibifu mkubwa katika maeneo mengi ya kusini mashariki mwa Afrika.

Kimbunga Idai, ambacho kiliupiga mji wa bandari wa Beira mchini Msumbiji Alhamisi iliyopita kabla ya kuingia maeneo ya ndani, kiliandamana na upepo mkali ulovuma kwa kasi na kuvunja majengo na kuyaweka hatarini maisha ya mamilioni ya watu. Rais wa Msumbiji Filipe Nyusi amesema kimbunga hicho kimewauwa zaidi ya watu 200 nchini Msumbuji lakini miili bado inaendelea kupatikana. Katika nchi jirani Zimbabwe, idadi rasmi ya vifo ni watu 98 lakini inatarajiwa kuongezeka kwa sababu mamia ya watu hawajulikani waliko. Wakati huo huo, msaada wa kimataifa umeanza kutolewa katika nchi za Msumbiji, Zimbabwe na Malawi kufuatia kimbunga hicho.

 

Chanzo; DW Swahili

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.