Star Tv

Watu wenye silaha wamewateka nyara wanafunzi 140 kutoka shule ya sekondari ya Bethel Baptist iliyoko Kaskazini Magharibi mwa Nigeria.

Ripoti hiyo ni kwa mujibu wa afisa wa shule aliyebainisha kwamba watu hao waliivamia shule hiyo na kisha kuwateka wanafunzi 140, ikiwa ni wimbi la karibuni kabisa la utekaji nyara unaowalenga wanafunzi nchini humo.

Watekaji hao walivunja uzio na kuingia katika shule ya sekondari ya Bethel Baptist ambayo ni ya bweni katika jimbo la Kaduna na kuondoka na wanafunzi hao.

Msemaji wa polisi katika jimbo hilo Mohammed Jalinge amethibitisha kutokea kwa tukio hilo lakini hakuweza kutoa maelezo zaidi kuhusu idadi ya wanafunzi waliochukuliwa mateka.

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.