Star Tv

Rais wa zamani wa Afrika Kusini Jacob Zuma, aliyetakiwa kujisalimisha gerezani ili kukitumikia kifungo cha miezi 15 kwa kuupuza amri ya Mahakama, amesema hatotii hukumu hiyo.

Wiki iliyopita, Mahakama ya Katiba ilimpa adhabu hiyo rais Zuma, kwa kutoheshimu agizo la Mahakama kutoa ushahidi kwa Tume iliyokuwa inachunguza madai ya ufisadi alipokuwa rais kati ya mwaka 2009 hadi 2018.

Akizungumza katika mkoa wa Kwa-Zulu Natal alikozaliwa, Zuma amewafananisha Majaji walitoa hukumu dhidi yake kama viongozi waliongoza taifa hilo wakati wa kipindi cha mapambano dhidi ya ubaguzi wa rangi.

Kiongozi huyo amesema kumtaka aende jela kwasasa ni sawa na kumpa hukumu ya kifo; "Hakuna haja ya mimi kwenda jela, kunifunga katika kipindi hiki, kwa umri wangu, ni sawa na kunipa hukumu la kifo"- Alisema Zuma.

Zuma mwenye umri wa miaka 79, alipaswa kujisalimisha gerezani siku ya Jumapili wiki iliyopita, lakini Mahakama imekubali kusikiliza rufaa ya kupinga kifungo hicho cha miezi 15.

Aidha wafuasi wa Zuma wameapa kutokubali kiongozi wao huyo wa zamani kufungwa.

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.