Star Tv

Baraza la Mawaziri nchini Ethiopia limetaja chama Tawala cha zamani cha Tigray Peoples Liberation Front (TPLF) party na kundi la Oromo Shene kama makundi ya kigaidi, Shirika la utangazaji wa Fana limeripoti.

Serikali ya nchini humo imelaumu mashirika hayo kwa kuhusika na mashambulio yaliofanywa katika maeneo tofauti yakiwalenga raia kwa lengo la kulemaza mageuzi yaliyoanzishwa na nchini humo katika kipindi cha miaka mitatu iliyopita.

Mwezi Novemba mwaka jana, Ethiopia ilianzisha oparesheni ya kijeshi Kaskazini mwa Jimbo la Tigray kuondoa madarakani TPLF kufuatia shambulio dhidi ya kambi za kijeshi katika eneo hilo.

Aidha, wakati Ethiopia inajiandaa kufanya uchaguzi mwezi Juni mwaka huu, Utawala wa Waziri Mkuu Abiy Ahmed umekumbwa na ghasia za kijamii zinazohusishwa na kundi la Shene.

 

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.