Star Tv

Rais wa zamani wa Afrika Kusini Jacob Zuma ametakiwa mpaka kufikia Jumatano awe amependekeza adhabu ambayo mahakama kuu ya nchi hiyo inapaswa kutoa ikiwa atapatikana na hatia ya kudharau.

Adhabu hiyo inahusiana na kupuuza kwake wito wa kufika mbele ya tume ya uchunguzi inayoongozwa na Jaji Ray Zondo kujibu tuhuma za ufisadi ambazo amekuwa akikana.

Mwezi Januari, mahakama ya katiba ya nchi hiyo ilimwamuru afike mbele ya tume hiyo, lakini akapuuza agizo hilo.

Mwezi uliopita, tume hiyo iliitaka mahakama imhukumu rais huyo wa zamani kwa miaka miwili, ili kuonesha uzito wa vitendo vyake akivyovitenda wakati akiwa madarakani.

Mahakama hata hivyo ilizuia uamuzi katika kesi hiyo, Ambapo wakati huo Zuma alisema haogopi kwenda gerezani ikiwa mahakama zitaamua hivyo.

Wakati huo huo mahakama ya rufaa Jumanne ilitetea uamuzi wa awali kwa serikali kupata pesa ambazo ilikuwa imezitumia kwa ada ya kisheria ya rais wa zamani.

Aidha, inakadiriwa kuwa serikali ililipa kati ya dola milioni moja na milioni 2.2 kama gharama katika kesi hiyo.

CHANZO:BBCSwahili

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.