Star Tv

Maafisa nchini Eritrea wamewaachilia kwa dhamana wafungwa 36 ambao wamekuwa mahabusu kwasababu ya imani yao.

Vyanzo vya habari vimeiambia BBC kuwa 14 kati ya wafungwa hao wamekuwa mahabusu kwa miaka minne iliyopita katika kisiwa cha Dahilik. Wengine 20 waliokamatwa mwishoni mwa mwezi uliopita wameachiliwa kwa dhamana.

Wafungwa wote wanatoka katika madhehebu ya Kiinjilisti na Kipentekoste.

Mwaka 2002 Eritrea ilianzisha sheria ambayo inazuia makanisa yote isipokuwa makanisa ya Orthodox, Katoliki na Lutherani, Aidha Waislamu wa madhehebu ya Sunni wanatambuliwa rasmi.

Serikali ya Eritrea imekuwa ikiwaachilia huru watu waliofungwa kwasababu za kidini.

Mwezi Septemba mwaka 2020, serikali ya Eritrea aliwaachilia mahabusu zaidi ya 20 ambapo walikuwa wamefungwa kwa miaka.

Mwezi Disemba, maafisa pia waliwaachilia wafuasi 28 wa kikundi cha Mashahidi wa Jehovah baada ya kutumikia kifungo cha jela kwa muda mrefu.

Wakristo wengi, bado wamebakia magerezani na wengine wamekuwa wakikamatwa mara kwa mara, kulingana na wanaharakati wa uhudu wa dini.

Serikali ya Eritrea inawashutumu Wakristo wa madhebebu ya Kipentekoste na kiinjilisti kwa kutumiwa na serikali za kigeni.

Eritrea, ambalo ni taifa lenye usiri, na la kijeshi kwa hali ya juu, imekuwa ikitawaliwa na Afwerki tangu ilipopata uhuru wak kutoka kwa Ethiopia mwaka 1993, bila uchaguzi au bunge na muswada wa katiba uliopo haujawahi kutekezwa.

Chanzo:BBCSwahili

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.