Star Tv

Rwanda na Kenya zimeanza kutoa chanjo kwa watoto ambapo wamebainisha kuwa sasa watoto nchini mwao wanastahili kupokea chanjo ya Pfizer huku nchi zote mbili zikianzisha kampeni za chanjo kwa rika hilo.

Rwanda itakuwa ikiwachanja watoto wenye umri wa kuanzia miaka 12 na kuendelea kuanzia Jumanne huku Kenya ikiwaruhusu wale wenye umri wa kuanzia miaka 15.

Rwanda ina idadi kubwa zaidi ya watu waliopata chanjo kamili katika Afrika Mashariki ikiwa na zaidi ya 20% ya jumla ya watu wote.

Mpango wa chanjo ya vijana wa Rwanda utashughulikia nchi nzima na wazazi au walezi wanapaswa kutia saini fomu za idhini kabla ya watoto wao kupewa chanjo.

Rwanda imebainisha kuwa itafanya kazi na shule kwa usambazaji na ukusanyaji wa fomu za idhini.

Nchini Kenya, Wizara ya Afya inatarajia kupokea dozi milioni nne za chanjo ya Pfizer kwenye kampeni yake ya kuwachanja vijana.

#ChanzoBBCSwahili

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.