Mamlaka nchini Uganda ilikatiza huduma za intaneti saa kadhaa kabla ya uchaguzi wa urais unaokumbwa na ushindani mkali kati ya Bobi Wine na Yoweri Museveni.
Kundi la ufuatiliaji wa masuala ya Itaneti NetBlocks liliandika kwenye Twitter yake kwamba nchi hiyo ilizima mitandao yote ya intaneti Jumatano saa moja usiku majira ya Afrika Mashariki.
Hatua hiyo ilifuatia agizo la serikali kufungia mitandao yote ya kijamii na programu tumishi za kutuma ujumbe.
Rais Yoweri Museveni alisema alifikia uamuzi huo kwa sababu Facebook ilifunga akaunti kadhaa zinazounga mkono chama tawala.
Mgombea wa urais,mwanamuziki aliyegeuka Bobi Wine aliandika katika Twitter yake kwamba huduma za intaneti zimekatizwa kama sehemu ya njama ya kuiba kura.
"Watu wa Uganda wako imara na hakuna jambo lolote litakatiza azma yao ya kikomesha utawala wa kiimla,"- aliongeza.
Shughuli za upigaji kura ilianza saa moja asubuhi ya leo Alhamisi Januari 14,2021, japo matokeo hayatarajiwi kutolewa kabla ya Jumamosi.
Kampeni za uchaguzi zilikumbwa na ghasia ambazo zilisababisha vifo vya makumi ya watu.
Bw. Museveni anagombea muhula wa sita baada ya kuwa madarakani kwa miaka 35.