Star Tv

Rais Uhuru Kenyatta ametangaza mipango ya kusaidia biashara na raia wa Kenya kusonga mbele katika kipindi hiki cha mdororo wa kiuchumi kwasababu ya janga la virusi vya corona.

Hayo yamejiri wakati rais akihutubia taifa kutoka Ikulu ya rais, Nairobi na kusema kwamba mipango hiyo itagharimu shilingi bilioni 53.7.

Katika hotuba yake, rais amesema pesa hizo zitagawanywa katika sekta muhimu kama vile miundombinu, elimu, biashara ndogondogo na za wastani, afya, kilimo, utalii, mazingira na viwanda vya uzalishaji.

Aidha, rais amesema kuwa taifa hilo haliwezi kuendelea kuchukua hatua za kusalia ndani milele;''Sisi kama serikali, kama serikali zingine, mataifa yote dunia zimeanza kuona, hatuwezi kuendelea kusema wakenya tukae nyumbani, hatuwezi kuendelea kusema tu wakenya msiende kufanya biashara, musiende makazi, namna hio".

Taifa hilo la Kenya inachukua hatua sawa na zile ambazo pia zimechukuliwa na nchi nyengine kama hatua ya kuchechemua uchumi unaoendelea kudidimia.

Uhuru amesema hayo wakati ambapo pia alitangaza kuwa Kenya maambukizi 31 ya virusi vya corona na kufikisha idadi hiyo hadi 1192.

Aidha ametoa wito kwa Wakenya ambapo amesema kuwa “Mimi sina shaka Wakenya tukishirikiana, tuungane pamoja, tutashinda huu ugonjwa, lazima tukumbuke ya kwamba jukumu ni letu sisi sote''.

Rais uhuru amewaambia wananchi wake kuwa ikiwa wataendelea kutekeleza masharti yaliyowekwa bila shaka taifa hilo litafanikiwa kukabiliana na changamoto zilizopo kwa sasa.

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.