Star Tv

Kamati Kuu ya CHADEMA imewafutia uanachama wabunge wanne wa chama hicho ambao ni Anthony Komu, Joseph Selasini,David Silinde na Wilfred Rwakatare.

Kufutwa uanachama kwa wabunge hao ni kutokana na kile kilichoelezea na Katibu Mkuu wa CHADEMA John Mnyika kuwa wamepoteza sifa ya uanachama wa Chama hicho.

Mnyika ameleeza kuwa Mbunge Anthony Komu na Joseph Selasini pamoja na kuwa wamejipotezea sifa ya uanachama wa CHADEMA, wamekuwa wakiuka maagizo ya Chama na hivyo Chama kimeazimia kuwafukuza uanachama.

Amesema Mbunge David Silinde na Wilfred Rwakatare sio tu kwamba wamekiuka agizo la Chama bali wamekuwa wakijitokeza kwenye vyombo vya habari kutoa maneno ya kashfa na kejeli dhidi ya maagizo ya Chama na Viongozi wa Chama, na hivyo kamati kuu ya CHADEMA imefikia uamuzi wa kuwafuta uanachama.

Pia amesema mjumbe wa Kamati Kuu CHADEMA, Mariamu Msabaha, ameshiriki kukiuka maagizo ya Chama, na wakati alitakiwa awe mfano, Kwakuwa amekwenda kinyume, amevuliwa nafasi zake zote ndani ya Chama na kubaki na Ubunge na atatakiwa ajieleze kwanini asichukuliwe hatua zaidi kwa kukiuka maagizo.

Aidha, Mnyika amesema kuhusu Wabunge wengine ambao wamekwenda kinyume na maagizo ya Chama hicho lakini hawajaonyesha utomvu wa nidhamu kwa kutoa kashfa kwa Chama na watatakiwa kujieleza ni kwanini wasichukuliwe hatua zaidi kwa kukiuka maagizo ya Chama.

 

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.