Star Tv

Serikali ya China imesema inajiunga na ubunifu wa ushirikiano wa kimataifa wa Shirika la Afya Duniani (WHO) kwa ajili ya kukabiliana na virusi hatari vya Corona.

Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya China Bi.Hua Chunying amesema kwamba serikali ya Beijing inakaribisha kujiunga na ubunifu wa ushirikiano wa kimataifa wa WHO kwa ajili ya kuharakishwa utafiti na uzalishaji wa vifaa vya afya vinavyohusiana na virusi vya Corona.

Chunying ameongeza kwamba serikali ya China inaunga mkono nafasi ya Shirika la Afya Duniani katika mapambano yake dhidi ya Corona na hivyo inakaribisha na kushiriki katika ubunifu na mapendekezo ya shirika hilo kwa lengo la kuharakisha shughuli za kufanyika utafiti, uzalishaji na kugawa chanjo na dawa za kukabili virusi vya Corona.

Kabla ya hapo, Tedros Adhanom Katibu Mkuu wa Shirika la Afya Duniani alitangaza kuzinduliwa kwa ubunifu wa ushirikiano wa kimataifa huku akionyesha matumaini kwamba China itajiunga na mpango huo.

 

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.