Star Tv

Maafisa wa afya Nchini China leo Mei 04,2020 Jumatatu wamebaini kuwa watu watatu wana maambukizi ya virusi vya Corona katika upande wa China Bara.

Licha kubaini uwepo wa watu hao walioambukizwa wametoa taarifa ya kutokuwa na kifo chochote kinachohusiana na ugonjwa huo ambacho.

Tume ya Kitaifa ya Afya nchini humo imesema kubainika kwa visa hivyo ni kwasababu wanafanya mikutano ya kila siku.

Maafisa hao wamesema watu wote watatu walioambukizwa virusi hivyo ni raia kutoka nchi za kigeni japokuwa hawajataja nchi hizo za kigeni ndio zipi.

Kwa jumla, kulingana na takwimu za tume hiyo, watu 82,880 wameambukizwa virusi vya Corona katika China Bara na kusababisha vifo vya watu 4,633. Huku takwimu zikionyesha kuwa zaidi ya watu milioni 3.5 wameambukizwa virusi vya Corona duniani.

China imeendelea kunyooshewa kidole cha lawama na Marekani kwamba ilipuuzia hatari ya ugonjwa wa Covid-19 na kusababisha nchi nyingi kuathirika na ugonjwa huo.

Mlipuko wa virusi vya corona unaosababisha ugonjwa wa Covid-19, ulitokea katika mkoa wa Hubei nchini China mwishoni mwa mwaka 2019.

Kufikia sasa kinachojulikana ni kuwa Covid-19, ni ugonjwa ambao unaothiri mfumo wa kupumua wa binadamu na wataalam wa Afya wanaeleza kuwa dalili zake ni pamoja na homa kali, kukohoa ambapo baada ya wiki moja au zaidi muathiriwa anaanza kukabiliwa na tatizo la kupumua.

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.