Star Tv

Ofisi ya Waziri Mkuu wa Uingereza Boris Johnson ya Downing Streeet imeeleza kuwa Waziri huyo amelazwa hospitalini ili kufanyiwa vipimo vya virusi vya Corona, siku 10 baada ya kukutwa na virusi vya ugonjwa huo.

Taarifa kutoka ofisi hiyo  zimeeleza kuwa Boris alikimbizwa katika hospitali moja ya mjini London siku ya Jumapili kutokana na kuonyesha dalili za virusi hivyo ikiwemo kiwango cha juu cha joto mwilini.

Kulingana na Mhariri wa BBC anayesimamia maswala ya kisiasa Laura Kuenssberg amesema Waziri Mkuu huyo anatarajiwa kulazwa hospitalini kwa kueendelea kufanyiwa vipimo vya kawaida.

Katika taarifa  ya msemaji wa ofisi ya Waziri Mkuu alisema:”Waziri Mkuu anaendelea kuwa na dalili za virusi vya corona siku chache baada ya kukutwa na virusi hivyo”.


Amesema pia Waziri Mkuu ameishukuru idara ya afya NHS kwa kazi nzuri na kuwaomba raia wa Uingereza kuendelea kufuata ushauri wa serikali wa kusalia nyumbani, ili kuwalinda wafanyakazi wa Afya na kuokoa maisha yao kwa ujumla.


Boris atafanyiwa vipimo kifuani na mapafu yake ili kufahamu iwapo amekuwa akipata tatizo la kupumua na pia huenda akafanyiwa vipimo vya moyo wake pamoja na vipimo vingine kuhusu kiwango cha oksijeni mwilini na kile cha seli nyeupe za damu , ini na figo kabla ya kutolewa hospitalini.


Waziri Boris alionekana hadharani mara ya mwisho akiwasifu wafanyakazi wa huduma ya Afya na wafanyakazi wengine muhimu katika nyumba yake huko Downing street siku ya Alhamisi jioni kabla ya kuongoza mkutano wa virusi vya corona akiwa karantini siku ya Ijumaa.

                                                             Mwisho.

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.