Star Tv

Rais wa Zanzibar na mwenyekiti wa baraza la mapinduzi Dokta Ali Mohammed Shein amewataka mawaziri wanaoshiriki mkutano wa kwanza wa SADC kuhakikisha wanapitisha mikakati imara itakayoweza kuondoa ama kupunguza madhara ya majanga.

Taarifa na Abdalla Pandu.

Rais Shein ametoa agizo hilo kufuatia nchi za jumuiya  ya kusini mwa Afrika SADC kupata maafa 160 ambayo yalipelekea zaidi ya vifo elfu 20 pamoja na kuathiri watu zaidi ya milioni 22.

Akifungua mkutano wa kwanza kwa mawaziri  wanahusika na masuala ya majanga kwa nchi za SADC Dkt. Shein amesema zaidi ya dola  bilioni tatu na milioni 700 zimetumika kwa kipindi cha 2015 mpaka 2018 kukabiliana na majanga yaliotokea hali ambayo imeathiri kwa kiasi kikubwa uchumi wan nchi za ukanda wa  SADC.

Dkt. Shein  amesema kufanyika kwa mkutano huo kumejenga matumaini kwa  wananchi wa nchi zote wanachama kwani majanga yamekuwa yakiwapa wasiwasi wa maisha yao na kupoteza watu pamoja na nguvu kazi ya nchi  hivyo kuna kila sababu ya washiriki  kutekeleza majukumu yao ili kupunguza au kuweza kukabiliana na pia kuvitambua viashiria vya majanga mapema .

Kutokana na mkutano huo kufanyika katika visiwa vya Zanzibar Dkt. Shein amezungumzia uzoefu wa athari za kimazingira kwa nchi za visiwa huku akiwakumbusha kuwa maafa makubwa waliopitia Zanzibar yaliyoyafanya serikali ya Zanzibar kuja na sera na mipango mikakati ambayo baadhi yake imeshatekelezwa.

Waziri wan chi afisi ya waziri mkuu  sera bunge kazi ajira vijana na watu wenye ulemavu Jenesta Mhagama amefafanua umuhimu wa mkutano huo katika kuandaa mifumo ya pamoja itakayosaidia nchi za SADC kujiweka tayari na kupunguza madhara ya maafa.

Huku katibu mtendaji wa sadec akifafanua agenda zilizoandaliwa ambazo kupitia mkutano huu wa mawaziri zitajadiliwa na kupitishwa ama vyenginevyo  zikilenga  mafanikio  ya kuziokowa nchi za jumuiya ya kusini mwa Afirika juu ya maafa na majanga mbali mbali.

Mkutano wa SADC ni wakwanza kufanyika Zanziabar na unatarajiwa utakuja na majawabu ya  busara katika mchakato mzima wa kujikinga na kukabiliana na maafa  yakiwemo yanayotokana na watu au ya kiasili kwa nchi zote wanachama.

                                                                    Mwisho

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.