Star Tv

Watu 73 walifariki jana nchini China bara kutokana na homa ya virusi vya corona, na kufikisha idadi ya vifo vya maradhi hayo kufika 563.

Zaidi ya asilimia 80 ya vifo na maambukizi nchini China vinatokea katika mkoa wa Hubei ilikoanzia homa hiyo hatari. Hadi wakati huu watu wawili wameuawa na maradhi ya hayo nje ya China Bara, mmoja nchini Ufilipino na mwingine katika kisiwa cha Hong Kong, na wahanga wote hao walikuwa wameutembelea mji wa Wuhan ambao ni chimbuko la ugonjwa huo.

Kitisho cha ugonjwa huo kinaripotiwa kuongezeka katika meli ya anasa ya kijapani iliyozuiliwa katika bandari ya Yokohama, ambapo wizara ya afya ya Japan inasema watu 20 kati ya 3,700 waliomo ndani ya meli hiyo iliyowekwa katika karantini, wamethibitika kuwa na maambukizi ya virusi vya corona.

                                                                                    Mwisho.

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.