Watu 73 walifariki jana nchini China bara kutokana na homa ya virusi vya corona, na kufikisha idadi ya vifo vya maradhi hayo kufika 563.
Zaidi ya asilimia 80 ya vifo na maambukizi nchini China vinatokea katika mkoa wa Hubei ilikoanzia homa hiyo hatari. Hadi wakati huu watu wawili wameuawa na maradhi ya hayo nje ya China Bara, mmoja nchini Ufilipino na mwingine katika kisiwa cha Hong Kong, na wahanga wote hao walikuwa wameutembelea mji wa Wuhan ambao ni chimbuko la ugonjwa huo.
Kitisho cha ugonjwa huo kinaripotiwa kuongezeka katika meli ya anasa ya kijapani iliyozuiliwa katika bandari ya Yokohama, ambapo wizara ya afya ya Japan inasema watu 20 kati ya 3,700 waliomo ndani ya meli hiyo iliyowekwa katika karantini, wamethibitika kuwa na maambukizi ya virusi vya corona.
Mwisho.