Leo tarehe 29/01 katika Bunge la 11 kikao cha pili, hati zilizowasilishwa mezani ni pamoja na taarifa ya kamati ya kudumu ya Bunge ya hesabu za Serikali kuhusu shughuli za kamati kwa mwaka 2019 ambazo zitawasilishwa na Mwenyekiti wa kamati ya kudumu ya Bunge ya Hesabu za serikali. Vile vile uwasilishwaji wa taarifa ya kamati ya kudumu ya Bunge ya Hesabu za serikali za mitaa kuhusu usimamizi wa matumizi ya fedha za umma katika serikali za mitaa kwa mwaka 2019,ambazo zitawasilishwa na mwenyekiti wa kamati ya kudumu ya Bunge ya hesabu za serikali za mitaa.