Star Tv

Wakazi wa kijiji cha Kitanda wilaya ya Namtumbo mkoani Ruvuma wamekumbwa na hofu ya kupata magonjwa ya tumbo kutokana na kunywa maji machafu yasiyofaa kwa matumizi ya binadamu.

 Kutokana na ukame wa maji uliopo kijijini hapo, wananchi na mifugo wanategemea kisima kimoja kupata maji ya kunywa jambo ambalo ni hatari kwa afya zao.

Wakazi hao wamesema adha ya upatikanaji wa maji inakwamisha shughuli ya maendeleo ikiwemo ujenzi wa nyumba bora kutokana na umbali wanakochota maji.

 Diwani wa kata ya Likuyu sekamaganga Kasimu Gunda amesema maji hayo hayafai lakini kutokana na shida waliyonayo wananchi wanalazimika kutumia.

 Kwa zaidi ya miaka 50 wananchi zaidi ya elfu tatu wa kijji cha Likuyu Seka wanaishi kwa maji ya kisima,mwaka 2012 serikali ilipeleka mradi wa maji ili kuwaondolea kero wananchi lakini ulisimama kwa zaidi ya miaka saba, serikali ya awamu ya tano imepeleka zaidi ya shilingi bilioni nne kuuendeleza ambapo hadi sasa upo katika hatua za mwisho.

 

                                                                      Mwisho

Latest News

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Urusi Kuchagiza Maendeleo Afrika kupitia Nishati ya Nuklia na Madini ya Urani
12 Aug 2023 10:07 - Kisali Shombe

ROSATOM, taasisi ya nishati ya nyuklia ya serikali ya Urusi ambayo iliwaalika zaidi ya waandishi wa habari 15 kutoka nch [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.